UCHAWI WAMPONZA MKE WA MTU
Author
Unknown
on
10:44:00 PM
in
-
Stori: Gordon Kalulunga, Mbeya
Uchawi!
Uchawi! Uchawi! Mwanamke ambaye ni mke wa mtu, aliyetajwa kwa jina moja
la Zai, mkazi wa Mtaa wa Ilolo, Kata ya Manga jijini hapa amenusurika
kuuawa baada ya kuponzwa na tuhuma za mambo ya ulozi au ushirikina.
Tukio hilo lililoshuhudiwa na Amani lilijiri maeneo hayo mwanzoni mwa
wiki hii ambapo wananchi takriban 200 waliitisha mkutano, wakitaka
kujichukulia sheria mkononi kwa kumpiga na kumchomea moto nyumba
mtuhumiwa huyo waliyedai kuchoshwa na maovu anayowafanyia.…
Stori: Gordon Kalulunga, MbeyaUchawi!
Uchawi! Uchawi! Mwanamke ambaye ni mke wa mtu, aliyetajwa kwa jina moja
la Zai, mkazi wa Mtaa wa Ilolo, Kata ya Manga jijini hapa amenusurika
kuuawa baada ya kuponzwa na tuhuma za mambo ya ulozi au ushirikina.
Tukio
hilo lililoshuhudiwa na Amani lilijiri maeneo hayo mwanzoni mwa wiki
hii ambapo wananchi takriban 200 waliitisha mkutano, wakitaka
kujichukulia sheria mkononi kwa kumpiga na kumchomea moto nyumba
mtuhumiwa huyo waliyedai kuchoshwa na maovu anayowafanyia.
Walidai
kuwa mwanamke huyo akimgusa mjamzito huwa mimba inaharibika huku
wanafunzi wanaotoka katika mtaa huo wakifika shuleni hushindwa kuona,
yote hayo yakihusishwa na mwanamke huyo.
Walisema
mwanamke huyo anatuhumiwa kujihusisha na matukio ya kishirikina tangu
ahamie mtaani miaka mitatu iliyopita ambapo walisema wakazi hao
walimuonya mapema kuhusu tabia hiyo baada ya kufuatilia historia ya
maeneo aliyowahi kuishi.
Kwa upande wake mumewe, Rubea (49),
alikanusha mkewe kuhusika na ushirikina huku akiwatupia lawama wananchi
hao kuwa wanaendekeza udini na hawapendi mtu wa dini nyingine tofauti na
ya kwao (haikutajwa ni dini gani).
Kwa
mujibu wa Mwenyekiti wa Mtaa wa Ilolo Kati, Ngambi Kulaba, wananchi hao
walikuwa wakimtuhumu yeye kuwa anamlinda mwanamke huyo lakini baada ya
kuona raia wamepagawa na kutaka kujichukulia sheria mkononi, ilimlazimu
kuwataarifu polisi ambao walifika na kukuta bonge la mtiti kisha
kumuokoa mwanamke huyo na kuondoka naye kwa usalama wake.
Post a Comment