Games

LATEST UPDATES

Monday, July 13, 2015

NILIONGEA NA SHETANI ILI NIWE TAJIRI 02

SIMULIZI YA KWELI: NILIONGEA NA SHETANI ILI NIWE TAJIRI
MTUNZI: STALLONE JOYFULLY

SEHEMU YA PILI
"Baba nakuheshimu kama baba yangu"
neno hilo likaniponyoka. Nilishuhudia mshangao wa
kuigiza katika uso wa Mzee Nyegezi. Sikujali niligeuka na
kutaka kuingia zangu chumbani. Alinishika tena mkono na
kuniambia
"hivi kama mama yako ameshakuambia, mimi si baba
yako mzazi; huoni kama hakuna kinachotuzuia sisi kuwa
wapenzi?" Alikuwa akicheka cheka kicheko kilichouudhi.
Alinisogelea na kuanza kunitomasa tomasa na mdomo
wake kuanza kuunganisha na papi zangu akiwa na nia ya
kutaka tubadilishane mate. Nilirudi nyuma baada ya
kumzaba kibao na kumuacha akiugulia maumivu na mimi
niliingia ndani haraka. Niliufunga mlango kwa ufunguo
nikimuacha nje akiropoka ropoka "mshenzi wewe huna
adabu nimekulea mimi siku zote leo unanivunjia adabu
mimi? Unanipiga kibao? Nitakuonesha mwanaizaya wewe"
alipotelea chumbani kwake huku akiendelea kubwatuka
___________

Niliamka asubuhi na mapema kwenda hospitali. Sikuona
umuhimu tena wa kumsubiri baba ikiwa ameanza
kunivunjia heshima. Amenivunjia heshima ya kunitaka
kimapenzi. Nilipanda daladala, kwa mwendo mrefu
ulioongezwa na msongamano, lakini nilifika. Mama
alikuwa ameamka, amekaa katika kitanda alicholazwa.
Baada ya salamu aliniuliza kiuchovu
"baba yako yuko wapi!?" sikumjibu. Sikujuwa cha kumjibu,
kwa kuwa sikutaka mama atambue yaliyotokea jana
usiku. Nilimpa uji niliotayarisha asubuhi. Aliunywa vibakuli
viwili na kutosheka. Aliniuliza tena. "ina maana baba yako
hajui kuwa nipo hospitali?"
nilimjibu "atakuja baadaye mama. Huenda yupo njiani"
mama akaniuliza tena "babu yako jana ulimuona tena?"
Nilimuhadithia yote kuanzia yule mtu aliyepewa lift na
baba na yote yaliyotokea na kutuambia kuhusu yeye
kukataa mimi kurithi mikoba ya babu. Mama naye
akaniambia
"jana usiku hospitali nzima iliona cha moto. Hapa
yenyewe leo nimelazimika kupewa discharge kutokana na
mauzauza yaliyokuwa yanatokea jana, yaani ni makubwa"
mama akaanza kunihadithia "Mwanangu jana wakati babu
yako anakuja alianza kuja katika umbile la mnyama" Mimi
mwili ulinisisimka na vinyweleo kunisimama. Ni nani
ambaye asingeogopa kusikia binadamu kawa paka?
Binadamu kuwa mnyama? Ni jambo la kushangaza.
Mama aliendelea "muuguzi mmoja aliyekuwa
akinihudumia alimpiga teke yule paka mwenye rangi ya
kijivu. Mimi sikuwa na habari kama yule alikuwa babu
yako. Alipomaliza kunifunga dripu ghafla alianza
kulalamika maumivu ya mguu. mguu ukazaa kichwa.
kichwa kichwa, kikazaa mauti ya ghafla" mama
alinyamaza kuruhusu pumzi ya kumeza mate. Mimi
nikabwatuka
"akafa? Mbona ghafla? Ilikuwaje?" mama alicheka
akaniambia
"mwanangu uchawi upo na una nguvu sana usipokuwa
mcha mungu. Nakumbuka yule muuguzi niliyemtambua
kwa jina la Rebecca wakati anampiga teke yule paka
aliropoka jambo" mimi nilikosa ustahimilivu, nikaropoka
tena "alisema nini?"
mama alitabasamu tena na kuniambia "usiwe na haraka
Bella ni hivi alisema 'hawa paka wengine ni wanga' Mimi
sikutilia maanani kwa kuwa nilimchukulia yule paka kama
mtu wa kawaida. Mara nilishangaa hospitali nzima ilijaa
paka wa kila aina. Madaktari na wagonjwa wenye nafuu
walijaribu kuwafukuza, lakini hawakufanikiwa. Paka hao
walikwishawauwa wagonjwa wawili na daktari mmoja.
Wale waliokuwa wanapambana na wale paka walikimbia
hovyo na wengine kuvunjika miguu. Kuna wengine
walionusuru roho zao. Lakini kati ya wale paka alijitokeza
paka wa kijivu yule aliyemuuwa muuguzi Rebecca na
kusimama karibu na kitanda changu" mimi macho
yakanitoka pima, nikamuuliza mama "sasa ulifanyaje"
mama aliendelea "nywele zilinisimama kama nimepigwa
na shoti ya umeme basi yule paka alijigeuza na kuwa
katika umbile la binadamu mbele yangu. niliogopa sana.
nilimsihi kwa machozi tele asinidhuru wala kuitoa roho
yangu. alikuwa ni babu yako Mzee Matonde. alicheka
sana na kuniambia, 'sijaja Kuitoa roho yako wala
kukudhuru. hili ni onyo la mwisho acha kumkataza Bella
kuirithi mikoba yangu'. kisha alinikumbusha ni jinsi gani
alivyoila nyama ya mwanaye wa kiume ambaye ni baba
yako. Pia kilikuwa ni kifo cha ghafla cha kuanguka bafuni.
Baba yako aliumia mguu tu. Mguu ukaoza ukaanza kutoa
harufu kali ya uvundo uliokera. Tukaliuza shamba la
mihogo, alipe pesa ya kitanda cha hospitali, pesa
hazikutosha. Akanishauri na kuniambia nisiliuze lile la
michikichi na fenesi kwa kuwa alishajua.
"umejua?" nilimuuliza mume wangu "umejua nini?" "baba
anataka kuniua"alipumzika baada ya kumeza donge zito
la uchungu. Chozi likamponyoka, likanyang'anya furaha
yake "najua atamsumbua mwanangu Bella lakini
nakuomba sana usiache kumuongoza mtoto wetu katika
maombi" mume wangu hakusubiri hata nimfute chozi kwa
kiganja changu wala hata hakutaka kuniaga, aliondoka
kimya kimya. Ukimya ulioniumiza na kunifanya nilie sana
na kusimama na msimamo wa kukataa kurithi mikoba ya
babu yako. Mzee Matonde alikuja siku moja nikiwa Eda
aliniambia kuwa 'nyama ya Jose tamu sana' nililia kwa
uchungu lakini sikuwa na la kumjibu. Alitokomea
alikokujua akicheka kifedhuli. Baada ya miaka mingi ndiyo
akarudi tena, aliniambia asingeshindwa kuitafuna mifupa
yangu kama nitaingilia harakati zake kama nilivyoingilia
kwa baba yako na kumsababishia kifo mume wangu.
Wakati Mzee Matonde anajaribu kunitisha, wale paka
waliyekuja na babu yako walitokezea na maiti za watoto
wadogo ambao walizaliwa kabla ya siku zao. sikujua nia
na madhumuni ya kuzichukua maiti zile. Babu yako alirudi
katika umbile la paka na kutoweka machoni mwangu
katika hali ya kufumba na kufumbua" wakati mama
anamaliza kunihadithia yaliyotukia jana, baba aliingia
akiwa na tabasamu la kuudhi. Mimi sikumjali akili yangu
ikawa imezama katika hadithi hiyo ya kusisimua hadithi
iliyonitingisha moyo wangu na kuanza kuogopa.
"Bella kumbe upo huku"
"niliamua kuwahi kumletea mama uji" nilimjibu kwa
karaha, kisha nilitoka nje. Baada ya muda mfupi naye
alitoka na kunieleza
"nimefurahi kwa kuwa, umenionesha umeanza kukuwa.
Hukumueleza kabisa kuhusu yaliyotokea jana? inabidi
nikupatie zawadi" sikumjibu. Japo yeye alicheka, mimi
nilinuna. Alielekea ofisini kwa daktari kulipia gharama za
matibabu ya mama, kisha tuliruhusiwa kurudi nyumbani.
mama alitakiwa apate muda mwingi wa mapumziko na
azimalize dawa zake za kunywa zitakazomsaidia
kuongeza damu, kutokana na upungufu wa damu alio
nao. Tulirudi nyumbani nikiwa na furaha ya mama kupata
nafuu. Mama alionekana akiwa na huzuni, mzee nyegezi
akiwa amepambwa na tabasamu la kishetani usoni
mwake.
Siku zikapita mpaka afya ya mama ilipotengemaa. Mimi
sikuona mauzauza yoyote tangu siku ile, mpaka leo siku
ya nane. Nilimuuliza mama "mama au babu kaamua
kutusamehe"
"we Bella omba Mungu tu mwanangu" mama aliamua
kunijibu kiuchovu. Nilicheka kicheko kisicho na ladha ya
kicheko. Nilimwambia tena mama "ameshindwa bwana na
madude yake. Mbona haji tena?" Mama akanikatiza "Bella
hufahamu wanapanga nini juu yetu.... Funga mdomo
wako" Nilinyamaza huku nikiwa na hakika babu hatokuja
tena. Hali ilikuwa shwari na siku saba alizozisema mama,
kuwa anaweza asifike basi zilipita. Nilifurahishwa na hali
hiyo na tuliishi kwa amani. Amani ya kutosumbuliwa na
babu lakini usisahau, Mzee Nyegezi hakuacha
kunisumbua. Alipopata upenyo wa kumtoroka mama
chumbani alinijia chumbani kwangu na kunitomasa
tomasa kimahaba. Nilipomtishia kupiga kelele, alikurupuka
kutoka chumbani kwangu na kurudi chumbani kwao. Siku
moja alipokuja chumbani kwangu mauzauza yakaibuka
tena haya yalichachamaa zaidi.
Baba aliingia kwa mwendo wake ule ule wa kuninyatia.
Hakutumia muda mwingi wala umbali mrefu kunifikia.
Alizipiga zile hatua ndefu ndefu zisizotoa sauti. Mimi
nilikuwa nimelala fofofo, hivyo sikusikia. Alipotaka kuitoa
khanga mwilini mwangu, nami nilishituka. Nilimuona baba
akiwa uchi wa mnyama. Alikuwa anatabasamu, tabasamu
la dharau. Nilipotaka kupiga kelele yeye alicheka kwa
nguvu alininong'oneza jambo
"mama yako ameifakamia wine niliyoweka madawa ya
kulevya. Utadhani hakuwahi kunywa wine tangu
amezaliwa?" alinicheka kwa kejeli. kisha aliongeza sauti
ya kicheko huku akibinya binya matiti yangu. wakati
akiendelea na mchezo huo mchafu ndipo niliusikia upepo
mkali uliovuma kwa nguvu. ulikuwa ni upepo mkali sana.
sauti ya kicheko cha dhihaka kikasikika kati kati ya
kicheko hicho. nilifahamu alikuwa ni babu. baba
alijidumbukiza ndani ya shuka kuificha aibu yake. alikuwa
anatetemeka sana. mimi nilijibanza ukutani pia nikiogopa
ile hali. mara mbele yetu akatokea joka kubwa lenye
vichwa viwili. alikuwa ni nyoka mwenye mabawa. siwezi
kusimulia kwa urahisi ni kiasi gani niliogopa lakini
nilishangaa kumuona Mzee Nyegezi amepoteza fahamu.
yule nyoka alizungumza
"nitakulinda siku zote. popote uendapo"
nilishajikojolea kwa uoga. Nilitetemeka haswa. yule nyoka
aliufahamu uwoga wangu aliniambia
"usiogope. mkuu wa ulimwengu huu amekuchagua"
kisha kama alivyokuja, aliondoka vile vile. Upepo wa kisuli
suli uliingia chumbani kwangu na kulimeza lile joka. Mimi
pia nilizimia kanga ikiwa mbali nami. Nguo ya ndani
ilisitiri maungo yangu huku mkono wa baba ukiwa kifuani
kwangu.
.........
sikumbuki nilipoteza fahamu kwa muda gani, ila
nilishituka kipindi ambacho kulikuwa kumeshakuchwa.
Baba bado alikuwa amelala pembeni yangu. Nilikuwa
nikiugulia maumivu ya kichwa. Maumivu ambayo,
yaliyogonga kama niliyetaka kuzimia tena au nilipigwa na
kitu kizito. Nilikumbuka usiku uliotisha. Usiku wa joka
kubwa lenye mabawa. Upepo wa kisuli suli ukalibeba lile
joka na kupotelea hewani. Hakika ilikuwa ni hali ya
kumfanya yeyote kuzimia. Ndiyo hapo niliona kitu cha
kushangaza mbele yangu. Mwili wa mama ukiwa
umekumbatia sakafu. Mama alikuwa amedondoka karibu
na mlango wa chumbani kwangu. Akiwa ameyalalia
mapovu yaliyomtoka mdomoni. Kiukweli nilishituka sana.
Sikujua nianze vipi kumsaidia mama ikiwa Mzee Nyegezi
naye alikuwa hajiwezi. Nilitoka nje, nikarudi ndani.
Nilipanda kitandani mara nikashuka. Nilimuita mama
lakini hakusikia. Nilimuinamia kwenye kifua chake na
kuyasikiliza mapigo yake ya moyo niliyasikia yakidunda
kwa mbali sana. Nikapata uhakika kuwa bado alikuwa
hai. Nilivaa nguo zangu haraka haraka. Nikafungua droo
katika kabati yangu kutazama kiasi cha pesa nilichokuwa
nacho. "shilingi elfu thelathini' zinatosha," nilijiambia.
Nilitoka mpaka eneo la hifadhi ya barabara, nilienda
kuchukua tax. Tax haikuchelewa, tulirudi nyumbani na
yule mzee ambaye alikuwa dereva, ndiye alinisaidia
kumbeba mama na kumuingiza ndani ya gari. Nilikuwa
nimechanganyikiwa sana. Nilichanganyikiwa baada ya
kufahamu kuwa, mama alipata mshituko wa kutuona mimi
na Mzee Nyegezi, tukiwa tumelala pamoja. Mzee Nyegezi
alikuwa kama alivyozaliwa, mimi nikiwa sina chochote
kifuani na nguo ya ndani pekee ilihifadhi maungo yangu.
Sikutaka niwe sababu ya kifo cha mama yangu. Sikutaka
kumuumiza mama. Wala sikutaka mama atoe chozi kwa
sababu yangu. Nilidondosha chozi nilipokuwa katika
kuwaza.
Yule dereva aliniuliza. "binti kuna nini?"
"acha tu mzee, naomba unipeleke lugalo"
"itakuwa elfu kumi"
"nimekuambia nipeleke Lugalo hospitali" Nilimjibu kwa
karaha. Sikujali kuhusu pesa, nilijali mama afike mapema
hospitali; apate matibabu. Nilikuwa nikimpepea mama
aliyelalia mapaja yangu, huku nikilia kwa uchungu. Nililia
huku nikimlaani mzee Nyegezi kwa tamaa zake. Mwendo
wa tax ulikuwa ukiridhisha. Mzee yule aliikimbiza tax
huku akipiga honi za hapa na pale. Japo alikuwa
akiendesha kwa kasi kama uwajuavyo madereva tax,
hakuacha kunisumbua kuniuliza hili na lile. Aliniuliza "na
Yule mwanaume aliyelala uchi pale kitandani ni nani?"
nilitamani nimtukane, ila nilimuheshimu. Sikumjibu kitu
niliendelea kuomba Mungu mama awe mzima. Foleni
ilimpisha na yeye kupita bila matatizo. Punde si punde
tulifika eneo la hospitali. Machela ikakimbizwa na
kumbeba mama. Mimi nilimlipa Yule babu na kumfuata
mama alipokuwa akipelekwa. Nilipofika katika wodi flani
ambayo sikuitambua kwa haraka nilisimamishwa.
"tafadhali naomba usubiri hapo nje" Muuguzi mmoja
alisema na mama kuingizwa sehemu fulani hivi na
kufunika pazia la kijani. Nilibaki nikiwa nimesimama.
Nilizunguka kila sehemu. Kulia nilitaka, maombi nikaona
yalichelewa. Kila muuguzi alipotoka katika chumba
alichoingizwa mama, mimi nilitoka mbio kumfuata.
"naomba unijuze hali ya mama"
"tafadhali kuwa na amani, amepata mshituko wa kawaida
yupo sawa" nilikaa kwenye benchi iliyopo katika baraza la
hospitali. Daktari aliyekuwa akimuhudumia mama, alitoka
akaniambia "wewe ndiye mwenye mgonjwa hapa?"
"ndiyo"
"nifuate ofisini" Nilimfuata ofisini nikiwa katika hali ya
uoga sana. Sikujuwa nini alikuwa anaenda kuniambia,
lakini sikupenda kupokea jibu lolote baya. Nilipoingia
baada ya kukaa, aliniambia. "ilikuwaje huyu mama
akafikia katika hali hii?"
"nahisi alipoteza fahamu baada ya kupata mshituko,
Daktari"
"hilo ndiyo jambo baya lililomkuta" Nilishituka sana
daktari aliposema hivyo. Nilianza kulia sikujua daktari
alimaanisha nini. Yeye alininyamazisha na kunieleza yote
sasa.
"sasa unalia nini? Nimeshakueleza tatizo kwani?"
Alinyamaza akavuta pumzi baada ya kumeza mate na
kuniambia. "huyu mwanamke hana tatizo lolote la
kimuonekano, ila ubongo wake umecheza na kusababisha
kumpotezea kumbukumbu mara kwa mara hivyo watu wa
karibu inabidi muizuie hali ya yeye kudondoka dondoka
kila mara"
"sawa dokta, ninaweza kumuona?"
"bila shaka"
Nilienda katika chumba ambacho daktari alinielekeza.
Chumba ambacho mama alikuwa amewekwa kama
mapumziko. Nilipomtazama mama, machozi yalikuwa
yakinitoka tu bila sababu. Nilijisikia vibaya sana kwa hali
aliyotukuta nayo na Mzee Nyegezi. Nilimsalimu na
alionesha kunikumbuka. "marahaba Bella"
Lakini hakuwa amechangamka wala hakuwa na furaha.
Niliona chozi likimponyoka na kushuka mpaka kwenye
mashavu yake. Nilmsogelea na kumwambia "mama
naomba nikueleze" akaniambia "huna haja ya kunieleza
lolote Bella inatosha"
"mama sivyo kama unavyofikiria mama" Nilimsihi
anisikilize, nilimuhadithia kila jambo lilivyokuwa mpaka
mimi na Mzee Nyegezi kuwa katika hali aliyotukuta nayo
asubuhi. Aliniambia "kwanini hukunieleza mapema?"
"niliogopa wewe ungegombana na baba"
mama hakuongea chochote mimi nilitoka katika kile
chumba na kwenda kwa daktari. Nililipa kila gharama za
uuguzi wa mama yangu na kuambiwa kuwa nimuache
kwanza mpaka mchana ndiyo nitaweza kuondoka naye.
Mama alitundukiwa dripu ya maji. Mimi nilirudi nyumbani.
Sikumkuta mzee Nyegezi katika chumba changu tena.
Nikatoka na kwenda jikoni. Ndipo nikasikia hatua za mtu
akinyata niliposimama, akaniziba mdomo.

*****
ITAENDELEA!!!
TOA MAONI YAKO!!!
Share This :

Post a Comment

 

Top