Games

LATEST UPDATES

Tuesday, February 12, 2013

RADIO FREE AFRICA KITANZINI KWA KANISA LA WASABATO NI BAADA YA KUTANGAZA TAARIFA ZISIZO ZA KWELI



Baadhi ya Waandishi wa habari wa Mkoa wa Mara wakiwa katika chumba cha mchungajiDaudi Makoye kwa ajili ya kwenda kusikilza wito walioitiwa na mchungaji huyo.

MWENYEKITI wa Kanisa la Waadventista wasabato Jimbo la Mara na Ukerewe (Mara Conference), Daudi Makoye amekanusha vikali mbele ya waandishi wa habari taarifa  iliyotolewa na Radio  Free Africa kuwa Mchungaji wa Kanisa hilo la Ukerewe, Emmanuel Tarara kuwa amebaka mtoto mwenye umri wa miaka minane na kwamba huyo si mchungaji wa kanisa hilo.


 
Na Thomas Dominick,
Musoma.

MWENYEKITI wa Kanisa la Waadventista wasabato Jimbo la Mara na Ukerewe (Mara Conference), Daudi Makoye amekanusha vikali taarifa  iliyotolewa na Radio  Free Africa kuwa Mchungaji wa Kanisa la Waadvetista wa Sabato la Ukerewe, Emmanuel Tarara kuwa amebaka mtoto mwenye umri wa miaka minane na kwamba huyo si mchungaji wa kanisa hilo.

Sambamba na kumtaka mtangazaji wa redio hiyo Jovinta Kaijage kukanusha mara moja na kuomba radhi kwa kanisa hilo na watanzania kwa ujumla la sivyo watamchukulia hatua yeye na chombo chake.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Kanisa la waadventisa wa sabato la Kamunyonge, Mchungaji Makoye  alisema kuwa taarifa hiyo iliyotangazwa juzi katika kipindi chake cha “Matukio” kinachotangazwa kuanzia saa moja ya asubuhi, ilitangazwa na mwandishi wake Jovinta Kaijage kutoka Ukerewe.


"Tunapenda kukanusha vikali taarifa hii kwa sababu hauna ukweli wowote Kanisa la Waadventista Wasabato kwa sasa ina wachungaji watatu katika wilaya ya Ukerewe.”alisema Mchungaji Makoye.

Aliwataja wachungaji wa Ukerewe ni pamoja na Mchungaji Elifamili Kashanga anayesimamia mtaa wa Mrutunguru, Mchungaji Kapete Mafuru anayesimamia mtaa wa Ilangara.

Mitaa mingine inasimamiwa na Mchungaji Zefa Ayugi anayesimamia mtaa wa Buhima na mtaa wa Nansio unasimamiwa na Mzee wa kanisa ndugu Staford Maiga anayekaimu nafasi ya mchungaji Daniel Muhono aliyehamia Mtaa wa Buturi hadi atakapopelekwa  mchungaji mwingine. 

Alisema kuwa kutokana na taarifa hizo waliwasiliana na Mzee wa kanisa, Staford Maiga wa Nansio ambaye walizungumza nae kwa simu juu ya jina hilo na kuthibitisha kuwa  Emmanuel Tarara hata si mshiriki wa kanisa hilo.

Aidha amewaomba  waandishi wa habari na hasa wa chombo kilihusika (RFA) kutoa taarifa sahihi iliyofanyiwa uchunguzi  na kuhakikishwa kisha kuutangaza kwa wananchi. 

“Waandishi wa habari ni watu waliiopewa  dhamana ya kuelemisha na kudumisha amani ya umma ya watanzania na kokote na kwamba  ni taarifa za uhakika tua nizo zinazosikika, hivyo  si vizuri kutoa taarifa isiyo sahihi na yenye malengo mbaya kwa  hisia za watu na inayoweza kuleta mfarakano na fitina katika jamii,”alisema.

Pia taarifa isitolewe ambayo inaweza kuleta picha mbaya au kupaka matope dhehebu na kuharibia sifa ya kanisa hivyo pamoja amemtaka Mwandishi huyo aombe radhi kwa jumuia ya kanisa la Waadventista Wasabato na watanzania wengine waliosikiliza habari hiyo  kurekebisha taarifa hiyo haraka.
Share This :

Post a Comment

 

Top