Games

LATEST UPDATES

Thursday, January 31, 2013

MTANGAZAJI WA REDIO WA TANZANIA AKAMTWA NA MADAWA YA KULEVYA NCHINI KENYA





Hivi karibuni mamlaka nchini Kenya zilikamata madawa ya kulevya aina ya heroin yenye uzito wa kilo 5.44.

Msemaji wa mamlaka ya mapato nchini Kenya (KRA) Kennedy Onyonyi amesema madawa hayo yalikamatwa yakiwa na mtanzaniaSaraphia Peter Shirima, Jan. 23 alipokuwa akijaribu kuvusha madawa hayo kupitia uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta.


Mamlaka hiyo imesema Saraphia sio mwanafunzi bali ni mtangazaji wa radio nchini Tanzania.Onyonyi alisema mtangazaji huyo ana kibali cha kuishi nchiini Sweden kwa miaka miwili kitakachoisha ” Nov. 28, 2014.

Madawa hayo yana gharama ya dola za kimarekani 150,000 ambapo mtuhumiwa huyo alikuwa akiyasafirisha kuyapeleka Budapest, Hungary.
Share This :

Post a Comment

 

Top